March 20, 2015

Mvua za Masika na Kadhia Yake Kwa Wanaoishi Mabondeni.


Licha  ya Mkuu wa mkoa wa  Dar es salaam Said Meck Sadick kuwataka wananchi wanaoishi mabondeni kuhama katika maeneo hayo kufuatia mvua zilizoanza  kunyesha jijini Dar es salaam wakazi hao wamegoma kuhama katika maeneo hayo.
Wakizungumza na Times FM hii leo mara baada ya mvua kunyesha, wakazi  hao wanaoishi maeneo ya mabondeni yanayohusisha Bonde la mto Msimbazi, Jangwani pamoja na Msasani  baadhi ya wananchi wamesema kwamba wanashindwa kuhama katika maeneo hayo kutokana na kutokuwa na kodi ya kulipia katika maeneo mengine yasiyo hatarishi.
Kwa mujibu wa Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu umebaini kuwa wakazi wanaoishi nyumba za mabondeni hulipia chumba kwa kuanzia shilingi elfu kumi na tano hadi elfu ishirini kwa mwezi. Yaani kwa upande wa elfu 15 kwa miezi  sita hulipia elfu tisini (90,000) na upande wa  elfu ishirini hulipia shilingi laki moja na elfu ishirini(120,000) kwa muda wa miezi sita.
Kwa upande wa nyumba zisizokuwa katika maeneo ya mabondeni hulipia kiasi cha kuanzia elfu hamsini (50,000) kwa mwezi ambayo ni sawa na shilingi laki tatu(300,000) kwa miezi sita.

Licha ya kodi kuwa bei ya chini kwa nyumba za  mabondeni sababu nyingine kubwa inayokwamisha wananchi hao kuhama wamesema kwamba ni serikali kushindwa kuboresha miundombinu ya maji  taka yanayozalishwa katika maeneo ya mabondeni  huku ikiwalazimisha kuhamia mabwepande ambako wanadai kuwa hakuna huduma za kijamii   hadi sasa.

No comments:

Post a Comment